Virai na Vishazi

Sentensi huwa na vifungu mbalimbali. Baadhi ya vifungu hivi ni vishazi na virai.

Virai (phrase)

Kirai ni fungu la maneno lisilokuwa na kitenzi.Phrase

Kuna aina nne za virai:

Kirai Nomino:

Kirai Nomino ni fungu la maneno katika sentensi lenye nomino (Kikundi Nomino/Kiima)

Kirai Kiwakilishi

Kirai Kiwakilishi ni fungu la maneno linalowakilisha nomino katika sentensi

Kirai Kivumishi

Kirai Kivumishi ni fungu la maneno katika sentensi linalotupa habari zaidi kuhusu nomino.

Kirai Kielezi

Kirai Kielezi ni fungu la maneno linaloelezea zaidi kuhusu kitenzi au kivumishi.

Vishazi (clause)

Kishazi ni sehemu ya sentensi yenye kitenzi. Kuna aina mbili za virai:

Kishazi Huru (Independent Clause)

Kishazi Huru huwa na maana kamili na kinaweza kujisimamia chenyewe kama sentensi.

Kishazi Tegemezi (Dependent Clause)

Kisha Tegemezi huhitaji kuunganishwa na kishazi kingine ili kuleta maana iliyokusudiwa. Aghalabu huwa na kirejeshi k.v amba-, -enye n.k