Fasihi Andishi

Fasihi Andishi ni aina ya sanaa ambayo hutumia maneno yaliyoandikwa kupitisha ujumbe. Ni sanaa inayopitishwa kwa njia ya maandishi

Tanzu za Fasihi Andishi

Kuna tanzu nne kuu za Fasihi Simulizi:

  1. Hadithi Fupi - kazi andishi ya fasihi isiyokuwa ndefu sana
  2. Riwaya - kazi andishi ya fasihi ambayo huwa ndefu kuliko hadithi fupi
  3. Tamthilia- kazi andishi ya fasihi inayowasilisha mchezo wa kuigiza
  4. Mashairi - mashairi yaliyochapishwa huwa chini ya fasihi andishi.

Sifa za Fasihi Andishi

  1. Hupitishwa kwa njia ya maandishi
  2. Ni mali ya mtu binafsi
  3. Haiwezi kubadilishwa
  4. Hutumia mbinu za lugha na mbinu za sanaa

Umuhimu wa Fasihi Andishi

  1. Kuhifadhi kazi ya sanaa katika maandishi
  2. Kukuza lugha
  3. Kuburudisha
  4. Kuelimisha
  5. Kukashifu tabia zisizoandamana na maadili ya jamii
  6. Kuonya, kuelekeza, kunasihi

Uchambuzi wa Fasihi Andishi

Unapochambua kazi ya fasihi andishi zingatia:

Aina ya Kazi Andishi

Wahusika

Maudhui na Dhamira

Mandhari

Mbinu za Lugha