Insha

Kuna aina mbili kuu za Insha.

Insha za ubunifu ni insha ambazo mwanafunzi huhitaji kubuni maudhui, mazingira, wahusika, na kadhalika kulingana na swali analorejelea. Insha hizi zinaweza kuwa za methali, mdokezo ama insha zenye mada ambazo hazina mtindo rasmi.

Insha za kiuamilifu ni maandishi yenye mtindo maalum na hutumika katika mazingira halisi kwa kuzingatia mtindo huo rasmi. Kwa mfano kumbukumbu, resipe, barua, ratiba, n.k. Ubunifu wa mwanafunzi hauwezi ukaathiri mtindo wa insha hizi. Kwa hivyo anchohitajika zaidi kuzingatia ni mtindo wa utunzi mada na hoja muhimu.