Msamiati wa Kazi

Huu ni msamiati wa watu wanaofanya kazi mbalimbali.

Mifano

  1. dobi:
    hufanya kazi ya kuosha nguo
  2. karani:
    anayeangalia matumizi ya pesa katika benki au kampuni fulani
  3. katibu:
    anayeweka rekodi za mambo na orodha mbalimbali katika kampuni au idara fulani
  4. kungwi:
    hufunza vijana jandoni
  5. mchuhuzi:
    anayeuza bidhaa kutoka nyumba hadi nyumba
  6. mfinyanzi:
    hufinyanga udongo kutengeza vyombo kama vyungu, n.k
  7. mhandasi:
    anayefanya kazi ya kuunda au kurekebisha injini/mashine mbalimbali
  8. mhasibu:
    mtu anayefanya kazi ya hesabu
  9. mhunzi:
    hufua vyuma
  10. mkatabi:
    anayeweka rekodi za vitabu katika maktaba, na kuwasaidia wanaotaka kuomba vitabu.
  11. tabibu:
    anayetibu watu
  12. topasi:
    kazi ya kuosha vyoo