Umoja na Wingi

Sentensi za Kiswahili zinaweza kubadilishwa kutoka kwa umoja hadi wingi, kulingana na ngeli yake. Baadhi ya ngeli hubaki sawia katika umoja na wingi.


Mifano ifuatayo itakuonyesha umoja na wingi wa sentensi katika ngeli mbalimbali.

Ngeli ya A-WA
1. Mtoto huyu ni mvivu sana. Watoto hawa ni wavuvi sana.
2. Mwizi aliyeiba ng'ombe wa mzee mkongwe amekamatwa na mwananchi. Wezi walioiba ng'ombe wa wazee wakongwe wamekamatwa na wananchi
Ngeli ya KI-VI
1. Kitabu chako kiko juu ya kitanda Vitabu vyenu viko juu ya vitanda
2. Chumba kile kidogo kimeangukia chungu Vyumba vile vidogo vimeangukia vyungu.
Ngeli ya LI-YA
1. Jani lile linaficha tunda kubwa ambalo limeiva Majani yale yanaficha matunda makubwa ambayo yameiva.
2. Jiko lolote lenye kaa moto litolewe nje Meko yoyote yenye makaa moto yatolewe nje.
Ngeli ya U-I
1. Mtaa huo hauna mti wowote Mitaa hiyo haina miti yoyote.
2. Huu ndio mto uletao maji katika mji wetu Hii ndiyo mito iletayo maji katika mito yetu.
Ngeli ya U-ZI
1. Ukuta mwingine umepigwa kwa upembe Kuta nyingine zimevunjwa kwa pembe.
2. Ubao mrefu uliokuwa kwenye ua wetu ulikatwa kwa upanga mweusi Ndefu ndefu zilizokuwa kwenye nyua zetu zilikatwa kwa panga nyeusi.
Ngeli ya I-ZI
1. Nyumba iliyo karibu na barabara ile imefungwa Nyumba zilizo karibu na barabara zile zimefungwa.
2. Ndoo yenye maji imewekwa juu ya mbao kubwa Ndoo zenye maji zimewekwa juu ya mbao kubwa.
Ngeli ya U-YA
1. Uyoga uliokuwa hapa umeoza. Mayoga yaliyokuwa hapa yameoza.
2. Mhindi wa kuchoma umeibiwa. Mahindi ya kuchoma yameibiwa.
Ngeli ya YA-YA
1. Mafuta na maji hayawezi kuchanganyika Mafuta na maji hayawezi kuchanganyika.
2. Damu ni nzito kuliko maji Damu ni nzito kuliko maji.
Ngeli ya I-I
1. Sukari imemwagika kwenye changarawe hii. Sukari imemwagika kwenye changarawe hii.
2. Ugali ni tamu lakini mboga haina chumvi. Ugali ni tamu lakini mboga haina chumvi.
Ngeli ya U-U
1. Uji uliopikwa kwa unga wa wimbi ni mtamu kuliko ule wa mtama. Uji uliopikwa kwa unga wa wimbi ni mtamu kuliko ule wa mtama.
Ngeli ya PA-PA
1. Mahali ambapo palipandwa maua panapendeza sana Mahali ambapo palipandwa maua panapendeza sana.
Ngeli ya KU-KU
1. Huku niliko hakuvutii kama kwangu Huku tuliko hakuvutii kama kwetu
2. Kukimbia huku kunachosha. Kukimbia huku kunachosha.
Ngeli ya MU-MU
1. Nyumbani humu mna giza totoro. Nyumbani humu mna giza tororo