Muundo wa Sentensi

Kiima, Kiarifa, Shamirisho na Chagizo

Sentensi huwa imeundwa na maneno mbalimbali. Vijenzi hivi vya sentensi ni Kiima, Kiarifa, Shamirisho na Chagizo

Angalia:


a id="KT_na_KN"

Kikundi Tenzi(KT) na Kikundi Nomino(KN)

Hizi ndizo sehemu mbili kuu katika sentensi. Kila kundi kikundi kinaweza kuwa na maneno mbalimbali. Tutayachangua haya zaidi katika uchanganuzi wa sentensi.

Kikundi Nomino (Kiima): KN

Ni sehemu wa sentensi yenye nomino. Pia kikundi nomino kinaweza kushirikisha kikundi kivumishi au kishazi tegemezi. k.m:

Kikundi Tenzi (Kiarifa): KT

Ni sehemu ya sentensi yenye kitenzi. Licha ya kitenzi, kikundi tenzi kinaweza kushirikisha kikundi kielezi au kikundi kivumishi. Aidha, kikundi tenzi kinaweza kuwa na kikundi nomino kama shamirisho kipozi au kitondo.

k.m:

Shamirisho

Shamirisho ni mtendwa au mtendewa katika sentensi. Ni sehemu ya sentensi inayowakilisha kitu kilichofanyiwa kitu. Kuna aina tatu za shamirisho.

Shamirisho Kipozi - (direct object)

Ni sehemu inayowakilisha nomino inayopokea kitendo hicho moja kwa moja. Mtendwa

Shamirisho Kitondo - (indirect object)

Huwakilisha ambayo kitendo kinafanywa kwa ajili yake au kwa niaba yake. Mtendewa

Shamirisho ala kitumizi

Hurejelea ala au kifaa kinachotumika kutekeleza kitendo hicho

Chagizo

Hutuelezea zaidi kuhusu kiima, kiarifa au shamirisho. Aghalabu chagizo huwa kielezi au kivumishi.