Nyimbo Katika Fasihi Simulizi

Nyimbo ni aina ya sanaa katika fasihi ambayo hutumia lugha teule, sauti na kiimbo maalum.

Aghalabu nyimbo hutumia ala za mziki kama vile ngoma. Nyimbo zinaweza kuimbwa na mtu mmoja au zaidi.

Wimbo hugawanywa katika beti na mishororo. Nyimbo nyingi huwa na kiitikio au mstari ambao hurudiwa rudiwa.

Sifa za Nyimbo

Umuhimu wa Nyimbo katika Fasihi Simulizi

Vipera/Aina za Nyimbo

Kulingana na Muundo:

Kulingana na Ujumbe/Maudhui:

Nyimbo za Ndoa

Nyimbo za harusi huimbiwa bwana na bibi harusi kuwapongeza na kuwapa heko kwa kufunga ndoa yao. Aidha nyimbo hizi huwapa wawili hao mawaidha ya kutunza familia na watoto wao ili waishi pamoja.

Nyimbo za Jandoni/Tohara

huimbwa na vijana wanapopashwa tohara. Nyimbo hizi huonyesha ushujaa, na kuashiria kutoka kwamba anayetahiriwa amekuwa mtu mzima sasa.

Hodiya/Wawe

Hizi ni nyimbo ambazo huimbwa na watu wanapofanya kazi ili kuwatia bidii wafanye kazi bila kuhisi machofu.

Kimai

Nyimbo za Mabaharia - Hizi ni nyimbo za wanabahari wanaposafiri baharini.

Nyimbo za Mazishi/Huzuni/Simanzi

Hizi ni nyimbo za kuliwaza na kuwapa pole walioachwa na marehemu. Nyimbo hizi huwapa matumaini waombolezaji.

Nyimbo za Kidini

Hizi ni nyimbo ambazo huimbwa kumsifia Mungu, kuomba au kutoa mafunzo ya kidini.

Nyimbo za Kisiasa

Hizi ni nyimbo za kuwasifia viongozi wa kisiasa

Nyimbo za Kizalendo

Nyimbo za huonyesha uzalendo kwa kusifia taifa/nchi

Nyimbo za Mapenzi

Katika nyimbo za mapenzi, mwimbaji huimba kwa kumsifia mpenzi wake hasa kwa urembo na tabia zake.