Ngeli za Kiswahili

Ngeli ni vikundi vya majina ya Kiswahili. Katika mfumo wa kisasa (na unaokubalika), ngeli huundwa kwa kuunganisha viambishi viwakilishi vya nomino.

Kwa mfano, neno kitabu. Tunasema, "Kitabu kimepotea - Vitabu vimepotea."

Kwa kuunganisha kiambishi "KI"(umoja) na VI(wingi), tunapata ngeli ya KI-VI. Ni muhimu kusisitiza kwamba tunazingatia viambishi, wala si silabi ya kwanza.

Hivyo basi, maneno yasioyoanza kwa KI-VI kama vile chama -vyama yatakuwa katika ngeli ya KI-VI kwa kuwa yanachukua kiambishi KI => (Chama kimevunjwa - Vyama vimevunjwa.) Vivyo hivyo, kunayo majina yanayoanza kwa KI-VI yasiyokuwa katika ngeli ya KI-VI maadam yanachukua viambishi tofauti. k.v: kijana => A-WA (kijana amefika- vijana wamefika).

Tumekuandalia majedwali matatu kukupa mukhtasari wa ngeli zote za Kiswahili na jinsi baadhi ya maneno/viambishi vinavyobadilika kutoka ngeli moja hadi nyingine.


a) Jedwali la kwanza linakupatia ngeli, maelezo yake, na mifano ya majina:

NGELIMAELEZOMIFANO
A-WA

Hii ni ngeli ya majina ya viumbe wenye uhai k.v watu, wanyama, ndege, wadudu, miungu, malaika n.k Majina mengi katika ngeli ya A-WA huanza kwa sauti M- kwa umoja na sauti WA- kwa wingi. Hata hivyo baadhi ya majina huchukua miundo tofauti.

mtu - watu
KI-VI

Ni ngeli ya majina ya vitu visivyo hai, yanayoanza kwa KI- au CH- (umoja); na VI- au VY- (wingi). Pia ngeli hii hujumuisha majina ya vitu vingine katika hali ya udogo. k.v kitoto.

kitu - vitu
LI-YA

Hujumuisha majina ya vitu visivyo hai pamoja na yale ya ukubwa k.v jitu. Majina yake huchukua miundo mbalimbali. Baadhi yake huchukua muundo wa JI-MA (jicho-macho), lakini yanaweza kuanza kwa herufi yoyote. Kwa wingi, majina haya huanza kwa MA- au ME-.

jani - majani
U-I

Huwakilisha majina ya vitu visivyo hai, yaanzayo kwa sauti M- (umoja) na MI(wingi).

mti - miti
U-ZI

Hurejelea majina ambayo huanza kwa U- (umoja) na huchukua ZI- kama kiambishi kiwakilishi cha ngeli katika wingi. Majina yenye silabi tatu au zaidi hubadilishwa kwa wingi kwa kutoa sauti /u/' k.v ukuta-kuta. Majina ya silabi mbili huongezewa /ny/ katika wingi. k.v ufa - nyufa

ukuta - kuta
I-ZI

Hutumiwa kwa majina yasiyobadilika kwa umoja wala kwa wingi lakini huchukua viambishi viwakilishi tofauti: I- (umoja) na ZI- (Wingi). Mengi yake huanza kwa sauti /u/, /ng/, /ny/, /mb/, n.k

nyumba - nyumba
U-YA

Ni majina machache mno yanayochukua kiambishi U(umoja) na YA(wingi).

uyoga - mayoga
YA-YA

Hii ni ngeli ya vitu visivyoweza kuhesabika (nomino za wingi). Hayana umoja. Mengi ya majina haya huanza kwa MA- lakini yanaweza kuchukua muundo wowote.

maji
I-I

Ni ngeli ya majina ya wingi ambayo huchukua kiambishi I- kwa umoja na pia kwa wingi. Majina haya hayana muundo maalum.

sukari
U-U

Majina ya nomino za wingi yanayoanza kwa sauti /u/ au /m/. Hayana wingi.

unga
PA-PA

Ni ngeli ya mahali/pahali - maalum.

mahali
KU-KU

Ngeli ya mahali - kwa ujumla. Aidha, hujumuisha nomino za kitenzi-jina

uwanjani
MU-MU

Ngeli ya mahali - ndani.

shimoni



b) Jedwali la pili linaangazia jinsi ngeli mbalimbali zinavyotumia "a-nganifu", viashiria na viashiria visisitizi.

NGELIA- UNGANIFUVIASHIRIAVIASHIRIA VISISITIZI
KARIBUMBALI KIDOGOMBALIKARIBUMBALI KIDOGOMBALI
A-WAwa
wa
huyu
hawa
huyo
hao
yule
wale
yuyu huyu
wawa hawa
yuyo huyo
ao hao
yule yule
wale wale
KI-VIcha
vya
hiki
hivi
hicho
hivyo
kile
vile
kiki hiki
vivi hivi
kicho hicho
vivyo hivyo
kile kile
vile vile
LI-YAla
ya
hili
haya
hilo
hayo
lile
yale
lili hili
yaya haya
lilo hilo
yayo hayo
lile lile
yale yale
U-Iwa
ya
huu
hii
huo
hiyo
ule
ile
uu huu
ii hii
uo huo
iyo hiyo
ule ule
ile ile
U-ZIwa
za
huu
hizi
huo
hizo
ule
zile
uu huu
zizi hizi
uo huo
zizo hizo
ule ule
zile zile
I-ZIya
za
hii
hizi
hiyo
hizo
ile
zile
ii hii
zizi hizi
iyo hiyo
zizo hizo
ile ile
zile zile
U-YAwa
ya
huu
haya
huo
hayo
ule
yale
uu huu
yaya haya
uo huo
yayo hayo
ule ule
yale yale
YA-YAyahayahayoyaleyaya hayayayo hayoyale yale
I-Iyahiihiyoileii hiiiyo hiyoile ile
U-Uwahuuhuouleuu huuuo huoule ule
PA-PApahapahapopalepapa hapapapo hapopale pale
KU-KUkwahukuhukokulekuku hukukuko hukokule kule
MU-MUmwahumuhumomlemumu humumumo humomle mle



c) Jedwali la pili linaangazia virejeshi(-o, amba-, -enye, -enyewe), ote, o-ote, ingi, ingine n.k kulingana na ngeli mbalimbali.

NGELIKIREJESHIO-REJESHI (AMBA-)ENYEENYEWEOTEO-OTEINGIINGINE
A-WAye
o
ambaye
ambao
mwenye
wenye
mwenyewe
wenyewe
wote
wote
yeyote
wowote
mwingi
wengi
mwengine
wengine
KI-VIcho
vyo
ambacho
ambavyo
chenye
vyenye
chenyewe
vyenyewe
chote
vyote
chochote
vyovyote
kingi
vingi
kingine
vingine
LI-YAlo
yo
ambalo
ambayo
lenye
yenye
lenyewe
yenyewe
lote
yote
lolote
yoyote
jingi
mengi
jingine
mengine
U-Io
yo
ambao
ambayo
wenye
yenye
wenyewe
yenyewe
wote
yote
wowote
yoyote
mwingi
mingi
mwingine
mingine
U-ZIo
zo
ambao
ambazo
wenye
zenye
wenyewe
zenyewe
wote
zote
wowote
zozote
mwingi
nyingi
mwingine
nyingine
I-ZIyo
zo
ambayo
ambazo
yenye
zenye
yenyewe
zenyewe
yote
zote
yoyote
zozote
nyingi
nyingi
nyingine
nyingine
U-YAo
yo
ambao
ambayo
wenye
yenye
wenyewe
yenyewe
wote
yote
wowote
yoyote
mwingi
mengi
mwingine
mengine
YA-YAyoambayoyenyeyenyeweyoteyoyotemengimengine
I-Iyoambayoyenyeyenyeweyoteyoyotenyinginyingine
U-Uoambaowenyewenyewewotewowotemwingimwingine
PA-PApoambapopenyepenyewepotepopotepengine
KU-KUkoambakokwenyekwenyewekotekokotekwingikwengine
MU-MUmoambamomwenyemwenyewemotemomotemengine