Hekaya

Hekaya ni hadithi ambazo huwa na mhusika mmoja mjanja au mwerefu kuliko wenzake. Mhusika huyu hutumia ujanja kujinufaisha kutoka kwa mhusika mwengine anayedanganyika kwa upesi. Kwa mfano, Hekaya za Abunuwasi, hadithi za sungura mjanja n.k

Sifa za Hekaya


  1. Huwa na mhusika mmoja mjanja anayewahadaa wenzake.
  2. Mhusika mjanja hunufaika kutoka kwa wengine japo hastahili.
  3. Ni hadithi fupi yenye funzo fulani



Umuhimu wa Khurafa


  1. Kuburudisha hadhira
  2. Kutoa mafunzo
  3. Kutahadharisha
  4. Kuelekeza na kunasihi
  5. Kupitisha muda



Mifano


  1. Hadithi za Sungura na Fisi
  2. Hadithi za Abunuwasi