Semi - Misemo na Nahau

Semi ni mafungu ya maneno yanayotumiwa kuleta maana nyingine badala ya maana halisi ya maneno yaliyotumika.

Kwa mfano tukisema mtu amegonga mwamba hatumaanishi kwamba amepiga jiwe kubwa kwa mkono au kwa kifaa chochote, bali tunamaanisha kwamba ameshindwa kuendelea katika jambo fulani.

Semi ni kipera cha tungo fupi katika fasihi simulizi; na hutumiwa katika aina nyingine za sanaa kama tamathali za lugha. Kuna fani mbili za Semi:

Umuhimu wa Semi

Mifano ya Nahau

NAHAU MAANA
Kupiga moyo konde kujituliza/kujiliwaza
Kujipa moyo kujiliwaza
Kupiga hatua kuendelea mbele
Kukata kamba kuaga dunia
Kupiga darubini kufanya uchunguzi
Kutupa macho kuangalia mbali
Kupigwa kalamu kufutwa kazi
Kuandaa meza kutayarisha chakula
Kugonga mwamba kutofanikiwa
Kwenda msalani kwenda chooni

Mifano ya Misemo

MSEMO MAANA
Mkono wa birika uchoyo
uzi na shindano ushirikiano
Shingo upande bila kupenda
kiguu na njia mtu asiyetulia mahali pamoja
Mdomo na pua karibu sana
Lila na fila mema na mabaya