Fasihi Simulizi ni utanzu wa fasihi ambao unawakilisha sanaa ya lugha inayopitishwa kutoka kwa kizazi hadi kizazi kwa njia ya maneno/masimulizi ya mdomo.
Sifa za Fasihi Simulizi
Hupitishwa kwa njia ya mdomo
Ufanisi wa sanaa katika fasihi simulizi hutegemea uwezo wa msimulizi, au wahusika
Masimulizi yake yanaweza kuathiriwa na mazingira, hisia na hali
Ni mali ya jamii. Hakuna mtu fulani anayemiliki sanaa katika fasihi simulizi.
Inaweza kubadilika kutoka kizazi hadi kizazi, au mazingira mbalimbali kwa sababu hutegemea kumbukumbu ya msimulizi.
Aghalabu huwa na funzo fulani
Umuhimu wa Fasihi Simulizi
Kuburudisha - Hufurahisha na kuchangamsha hadhira
Kunasihi- kutolea mawaidha na kuonyesha mwelekeo unaotarajiwa katika jamii
Kuelimisha watu kuhusu vitu mbalimbali hasa mazingira yao
Kutambulisha jamii - jamii mbalimbali husifika kutokana na sanaa zao katika fasihi simulizi kama vile nyimbo
Kuhifadhi na kudumisha utamaduni wa jamii
Kuunganisha watu - huleta watu pamoja
Kukuza lugha - fasihi huimarisha lugha kwa kuwa hutumia mbinu mbalimbali za lugha.
Kuliwaza - hutoa huzuni na kuleta matumaini.
Kupitisha muda - wakati mwingine fasihi simulizi hutumika kupitisha muda.