Aina za Viwakilishi
Viwakilishi vya Nafsi
Viwakilishi hivi hutumika kwa niaba ya nafsi kwa umoja na kwa wingi.NAFSI | UMOJA | WINGI |
Nafsi ya Kwanza | Mimi | Sisi |
Nafsi ya Pili | Wewe | Ninyi/Nyinyi |
Nafsi ya Tatu | Yeye | Wao |
- Sisi tuliwatangulia nyinyi kufika hapa.
- Mimi si mjinga kama vile yeye anavyofikiria
Viwakilishi Viashiria
Viwakilishi viashiria (vionyeshi) hutumika badala ya nomino kwa kutumia kuonyesha nomino inayorejelewa bila kuitaja.- Hiki hakina maandishi yoyote.
- Hao hawajui tofauti ya viwakilishi na vivumishi
- Tumekuja hapa ili kuwaburudisha kwa nyimbo tamu tamu.
Viwakilishi Visisitizi
Husisitiza nomino inayowakilishwa kwa kurudiarudia kiashiria chake.- Zizi hizi ndizo zilizovunjika wiki jana
- Yule yule aliyekamatwa juzi, ameiba tena.
Viwakilishi vya Sifa
Husimama badala ya nomino kwa kurejelea sifa yake.- Vyekundu vimehamisha
- Warembo wamewasili.
- Kitamu kitaliwa kwanza.
Viwakilishi vya Idadi
Hutumika kusimama badala ya nomino kwa kurejelea idadi yake. a) Idadi Kamili- hutumia nambari kuelezea idadi ya nomino.- Wawili wamepigwa risasi polisi leo jioni.
- Alimpatia mtoto wake hamsini kununua chakula
- Tutazungumza na wachache kabla ya kuanzisha maonyesho yetu.
- Kadhaa zimeripotiwa kupotea.
Viwakilishi Viulizi
Viwakilishi viulizi hutumika kwa niaba ya nomino katika kuulizia swali.Baadhi ya viwakilishi viulizi huchukua viambishi vya ngeli
- Vingapi vinahitajika? - kuulizia idadi
- Zipi zimepotea?
- Gani imefunga bao hilo?
- Wapi hapana majimaji?
- Yule mvulana alikupatia nini?
- Uliongea naye vipi? - kuulizia namna
Viwakilishi Vimilikishi
Viwakilishi hivi hurejelea nomino kwa kutumia vimilikishi.- Kwetu hakuna stima.
- Lake limekucha.
- Zao zimeharibika tena
Viwakilishi Virejeshi (O-Rejeshi)
Hutumia O-rejeshi kurejelea na kusimamia nomino- Ambalo lilipotea limepatikana.
- Ambaye hana mwana, aeleke jiwe
Viwakilishi Vya A-Unganifu
Huwakilishi nomino kwa kutaja kinachomiliki nomino hiyo. Huundwa kwa kuambatanisha kiambishi cha nafsi/ngeli pamoja na kiambishi -a cha a-unganifu, kisha nomino nyingine- Cha mlevi huliwa na mgema
- Za watoto zitahifadhiwa.