Vihusishi ni maneno yanayotuarifu zaidi kuhusu uhusiano wa nomino na mazingira yake.
Aina za Vihusishi
Vihusishi vya Mahali
| mbele ya, nyuma ya |
Kuna mzoga '_'nyuma ya'_' jengo hilo. |
| chini ya, juu ya |
Joto lilipozidi, watoto waliketi '_'chini ya '_' mti ule. |
| kando ya |
'_'Kando ya '_' mito ya Babeli ndipo tulipoketi. |
| karibu na, mbali na |
Fisi aliambiwa asile mifupa '_'karibu na'_' mtoto yule. |
Vihusishi vya Wakati
| kabla ya |
Ni vizuri kusali '_'kabla ya'_' kula chakula. |
| baada ya |
Watoto safi hupiga meno mswaki '_'baada ya'_' kila mlo. |