Kihisishi |
Mfano katika Sentensi |
Hisia |
Lo! |
Lo! Maajabu ya Musa haya! |
mshangao |
Salaale!, Masalaale! |
Salaale! Angalia watu wote hawa waliofika mahali hapa! |
mshangao |
Kumbe! |
Nilidhani wewe ni rafiki yangu. Kumbe! |
mshangao |
Po! |
Sijawahi kuona kijana mjeuri kama wewe. Po! |
hasira |
Ng'o! |
Omba msamaha utakavyo, lakini unachoka bure. Ng'o! |
kiburi |
Hata! |
Bwanake hakumwachia chochote! Hata! |
kusifia, kupuuza |
Akh!, Aka! |
Mtoto mpumbavu huyu! Akh! |
hasira, kukashifu |
Ah! |
Ah! Sikuyaamini macho yangu. |
mshangao |
Ala! |
Ala! Umefika tayari! |
mshangao |
Haha! |
Haha! Umenivunja mbavu, bwana! |
kicheko |
Ehee!, Enhe! |
Enhe! Endelea, ninaipenda sana hadithi hiyo! |
kuitikia |
Hmmm! |
Hmmm! Chakula kitamu hicho! |
kuitikia, kusifia |
Ebo! |
Ebo! Tabia gani hiyo. |
kukashifu, hasira |
Kefule! |
Kefule! Umenifedhehesha sana. |
hasira |
Wee! |
Katamu alinegua kiuno na kucheza kwa madaha. Wee! Wavulana wakaduwaa. |
kusifia |
La!, Hasha! |
La! Sitaki kusikiliza upuuzi wako tena. |
kukataa |
Hoyeee! |
Wamama wote, hoyee! Hoyee! |
kushangilia |
Huraa! |
Huraa! Tumeshinda. |
kushangilia |