Uainishaji wa Neno

Kuainisha ni kugawa neno katika viambishi vyake mbalimbali. Tunapoainisha neno, tunaonyesha mzizi wa neno pamoja na viambishi vyote vilivyofungamanishwa kuunda neno hilo.


Angalia:


Mifano:

Ainisha maneno yafuatayo:

  1. nitasoma → ni-ta-som-a
    {
    ni → kiambishi kiwakilishi cha nafsi ya kwanza umoja
    ta → kiambishi kiwakilishi cha wakati ujao
    som → shina la kitenzi cha kusoma
    a → kiishio
    }
  2. walipozipata → wa-li-po-zi-pat-a
    {
    wa → kiambishi kiwakilishi cha nafsi ya pili wingi
    li → kiambishi kiwakilishi cha wakati uliopita
    po → kiambishi kiwakilishi cha po ya wakati au cha ngeli ya mahali PO
    zi → kiambishi kiwakilishi cha kitendwa, ngeli ya I-ZI wingi
    pat → shina la kitenzi cha kupata
    a → kiishio
    }
  3. vimeshikamana → vi-me-shik-aman-a
    {
    vi → kiambishi kiwakilishi cha ngeli ya KI-VI wingi
    me → kiambishi kiwakilishi cha wakati uliopita muda mfupi
    shik → shina la kitenzi cha kupata
    aman→ kiambishi kiwakilishi cha kauli ya kutendamana
    a → kiishio
    }
  4. mnayemkimbilia → m-na-ye-m-kimbi-li-a
    {
    m → kiambishi kiwakilishi cha nafsi ya pili wingi
    na → kiambishi kiwakilishi cha wakati uliopo
    ye → kiambishi kirejeshi cha nafsi ya tatu
    m→ kiambishi kiwakilishi cha mtendewa, nafsi ya tatu umoja
    kimbi → mzizi wa kitenzi cha kukimbia
    li → kiambishi kiwakilishi cha kauli ya kutendea
    a → kiishio
    }
  5. yakimwagika → ya-ki-mwag-ik-a
    {
    ya → kiambishi kiwakilishi cha ngeli ya YA-YA
    ki → kiambishi kiwakilishi cha KI-ya masharti au au cha KI-ya kuendelea
    mwag → mzizi wa neno mwaga
    ik→ kiambishi kiwakilishi cha kauli ya kutendeka
    a → kiishio
    }
  6. hawakukushibisha → ha-wa-ku-ku-shib-ish-a
    {
    ha → kiambishi kiwakilishi cha kukanusha
    wa → kiambishi kiwakilishi cha nafsi ya tatu wingi
    ku → kiambishi kiwakilishi cha kukanusha wakati uliopita
    ku → kiambishi kiwakilishi cha nafsi ya pili mtendewa
    shib → mzizi wa kitenzi cha kushiba
    ish→ kiambishi kiwakilishi cha kauli ya kutendesha
    a → kiishio
    }
  7. lililolililia → li-li-lo-li-li-li-a
    {
    li → kiambishi kiwakilishi cha ngeli ya LI-YA umoja
    li → kiambishi kiwakilishi cha wakati uliopita
    lo → kiambishi kirejeshi cha ngeli ya LI-YA umoja
    li→ kiambishi kiwakilishi cha mtendewa, ngeli ya LI-YA
    li → shina la kitenzi cha kulia
    li → kiambishi kiishio cha kauli ya kutendea
    a → kiishio
    }