Fasihi Andishi ni aina ya sanaa ambayo hutumia maneno yaliyoandikwa kupitisha ujumbe. Ni sanaa inayopitishwa kwa njia ya maandishi
Tanzu za Fasihi Andishi
Kuna tanzu nne kuu za Fasihi Simulizi:- Hadithi Fupi - kazi andishi ya fasihi isiyokuwa ndefu sana
- Riwaya - kazi andishi ya fasihi ambayo huwa ndefu kuliko hadithi fupi
- Tamthilia- kazi andishi ya fasihi inayowasilisha mchezo wa kuigiza
- Mashairi - mashairi yaliyochapishwa huwa chini ya fasihi andishi.
Sifa za Fasihi Andishi
- Hupitishwa kwa njia ya maandishi
- Ni mali ya mtu binafsi
- Haiwezi kubadilishwa
- Hutumia mbinu za lugha na mbinu za sanaa
Umuhimu wa Fasihi Andishi
- Kuhifadhi kazi ya sanaa katika maandishi
- Kukuza lugha
- Kuburudisha
- Kuelimisha
- Kukashifu tabia zisizoandamana na maadili ya jamii
- Kuonya, kuelekeza, kunasihi
Uchambuzi wa Fasihi Andishi
Unapochambua kazi ya fasihi andishi zingatia:Aina ya Kazi Andishi
- Tambua aina au kipera cha kazi andishi ikiwa ni riwaya, hadithi fupi au tamthilia
Wahusika
- Tambua wahusika katika kazi hiyo ya fasihi
- Fafanua sifa za kila mhusika kwa kutumia vivumishi au virai vivumishi vinavyolingana na hulka za mhusika huyo.
- Aidha, unapaswa kuyakinisha sifa hizo kwa kutolea mifano kutoka kwenye hadithi
- Taja aina ya wahusika
Maudhui na Dhamira
- Maudhui - ni nini kinachofanyika?
- Dhamira - lengo/kusudi la kazi hiyo ni nini?
Mandhari
- Hadithi inafanyika katika mazingira gani?
- Mazingira hayo yanachangia vipi katika kisa hicho au sifa za wahusika?
- Msanii ameunda hali gani? (hisia, n.k)
Mbinu za Lugha
- Taja kwa kutolea mifano, fani za lugha zilizotumika ili kuifanya lugha iwe ya kuvutia zaidi
- Fafanua mbinu za sanaa zilizotumika na utaje mifano mwafaka