Msamiati wa hesabu/hisabati unaangazia: majina mbalimbali ya tarakimu/nambari; kuandika tarakimu kwa herufi.maneno; tarakimu za kiarabu; akisami (fractions) na asilimia (percentages).
Tumekuandalia:
- Nambari za Kimsingi (0-9) Kiswahili na Kiarabu
- Kumi na (11-19) Kiswahili na Kiarabu
- Makumi/Ukumi (10-90)
- Akisami (fractions)
- Mifano Kadhaa
NAMBARI ZA KIMSINGI
Haya ni majina ya tarakimu mbalimbali zinapoandikwa kwa herufi (badala ya nambari) yenye asili ya Kiswahili/Kibantu na pia yale yenye asili ya Kiarabu. Pia, tumeongezea majina ya makumi mbalimbali (10-90)
TARAKIMU |
KISWAHILI |
KIARABU |
0 |
sufuri |
sufuri |
1 |
moja |
wahed |
2 |
mbili |
thenini |
3 |
tatu |
thelatha |
4 |
nne |
aroba |
5 |
tano |
hamsa |
6 |
sita |
sita |
7 |
saba |
saba |
8 |
nane |
themania |
9 |
tisa |
tisa |
KUMI NA
Majina ya ya tarakimu kutoka (11-19) kwa Kiswahili na kwa Kiarabu.
10+ |
KISWAHILI |
KIARABU |
11 |
kumi na moja |
edatashara |
12 |
kumi na mbili |
thenashara |
13 |
kumi na tatu |
thelathashara |
14 |
kumi na nne |
arobatashara |
15 |
kumi na tano |
hamsatashara |
16 |
kumi na sita |
sitatashara |
17 |
kumi na saba |
sabatashara |
18 |
kumi na nane |
themantashara |
19 |
kumi na tisa |
tisatashara |
MAKUMI
Kuandika tarakimu mbalimbali katika hali ya ukumi. (11-99).
*10 |
JINA |
MFANO |
# |
KISWAHILI |
KIARABU |
10 |
kumi |
12 |
kumi na mbili |
thenashara |
20 |
ishirini |
27 |
ishirini na saba |
saba wa ishirini |
30 |
thelathini |
32 |
thelathini na mbili |
thenini wa thelathini |
40 |
arobaini |
42 |
arobaini na mbili |
thenini wa arobaini |
50 |
hamsini |
52 |
hamsini na mbili |
thenini wa hamsini |
60 |
sitini |
61 |
sitini na moja |
wahed wa sitini |
70 |
sabini |
76 |
sabini na sita |
sita wa sabini |
80 |
themanini |
89 |
themanini na tisa |
tisa wa themanini |
90 |
tisini |
93 |
tisini na tatu |
thelatha wa tisini |
AKISAMI
Akisami hutumiwa kuonyesha sehemu ya kitu kizima. Kwa mfano, ukigawa kilo moja kwa visehemu vinne vinavyotoshana,
kila kisehemu kitakuwa na uzani wa robo kilo ( sehemu ya nne au moja kwa nne ) ya kilo.
1/# |
JINA |
MFANO |
1/2 |
nusu |
1/2 |
nusu |
moja kwa mbili |
1/3 |
thuluthi |
2/3 |
thuluthi mbili |
mbili kwa tatu |
1/4 |
robo |
2/4 |
robo mbili |
mbili kwa nne |
1/5 |
humusi |
3/5 |
humusi tatu |
tatu kwa tano |
1/6 |
sudusi |
4/6 |
sudusi nne |
nne kwa sita |
1/7 |
subui |
6/7 |
subui sita |
sita kwa saba |
1/8 |
thumuni |
7/8 |
thumuni saba |
saba kwa nane |
1/9 |
tusui |
3/9 |
tusui tatu |
tatu kwa tisa |
1/10 |
ushuri |
6/10 |
ushuri sita |
sita kwa kumi |
1/100 |
asilimia |
72/100 |
asilimia sabini na mbili |
sabini na mbili kwa mia moja |
MIFANO ZAIDI
Andika nambari zifuatazo kwa maneno/herufi:
- 3 - tatu
- 952 - mia tisa hamsini na mbili
- 680 - mia sita themanini
- 4521903 - milioni nne, na mia tano ishirini na moja elfu, na mia tisa na tatu
- 556100016 - mia tano hamsini na sita milioni, na mia moja elfu, na kumi na sita
Andika tarakimu zifuatazo kwa nambari
- sufuri - 0
- mia tatu ishirini na mbili - 322
- sabini na tatu elfu, na mia nane hamsini na tano - 73855
- mia tano sabini na nane elfu, na mia tatu hamsini na tisa - 578359
- mia sita tisini na sita milioni, na mia tisa tisini na nane elfu, na mia saba ishirini na tatu - 696998723
Andika akisami zifuatazo kwa maneno
- 240/295 - mia mbili arobaini kwa mia mbili tisini na tano
- 41/45 - arobaini na moja kwa arobaini na tano
- 26/51 - ishirini na sita kwa hamsini na moja
- 59/74 - hamsini na tisa kwa sabini na nne
- 1/3 - thuluthi