Maghani Katika Fasihi Simulizi

Maghani ni tungo zinazotolewa kwa kughanwa (nusu kuimbwa nusu kukaririwa) Maghani yanaweza kuambatanishwa na ala za muziki au kughanwa kwa mdomo tu.

Aina za Maghani

Zipo fani mbali mbali za maghani ambazo zimeainishwa katika tanzu mbili kuu:

a id="masimulizi"

Maghani ya Masimulizi

Lengo la maghani ya aina hii ni kusimulia kisa fulani, historia, n.k.

Kuna fani mbili za Maghani ya Masimulizi:

a) Tendi

Tendi ni ushairi mrefu unaosimulia matukio ya kishujuaa. Tendi zinaposimuliwa huandamana na ala za muziki.

Sifa za Tendi:

b) Rara

Hizi ni hadithi fupi za kishairi zenye visa vya kusisimua, zinazosimuliwa zikiambatanishwa na ala za muziki. Aghalabu hughanwa na watoto; na hutumika kama michezo ya watoto.

Sifa za Rara


a id="kawaida"

Maghani ya Kawaida (Sifo)

Maghani ya Kawaida ni maghani yanayosifia mtu, kitu au hali katika jamii

a) Majigambo au Kivugo

Haya ni maghani ambayo mtunzi hujisifia (kujigamba) namna alivyo hodari katika nyanja fulani. Tungo hizi hutumia chuku na maneno ya kejeli kuwadunisha wapinzani wa mtunzi.

Sifa za Majigambo

b) Tondozi

Tondozi ni aina ya sifo ambayo husifia watu mashuhuri katika jamii kama vile viongozi

Sifa za Tondozi

Pembezi

Pembezi ni maghani ya kumsifu mpenzi.

Sifa za Pembezi

ii) Pembezi - tungo za sifa. Zinaweza kusifia kundi fulani la watu, wanyama, njaa, mvua, n.k