Nyimbo za harusi huimbiwa bwana na bibi harusi kuwapongeza na kuwapa heko kwa kufunga ndoa yao. Aidha nyimbo hizi huwapa wawili hao mawaidha ya kutunza familia na watoto wao ili waishi pamoja.
Nyimbo za Jandoni/Tohara
huimbwa na vijana wanapopashwa tohara. Nyimbo hizi huonyesha ushujaa, na kuashiria kutoka kwamba anayetahiriwa amekuwa mtu mzima sasa.
Hodiya/Wawe
Hizi ni nyimbo ambazo huimbwa na watu wanapofanya kazi ili kuwatia bidii wafanye kazi bila kuhisi machofu.
Kimai
Nyimbo za Mabaharia - Hizi ni nyimbo za wanabahari wanaposafiri baharini.
Nyimbo za Mazishi/Huzuni/Simanzi
Hizi ni nyimbo za kuliwaza na kuwapa pole walioachwa na marehemu. Nyimbo hizi huwapa matumaini waombolezaji.
Nyimbo za Kidini
Hizi ni nyimbo ambazo huimbwa kumsifia Mungu, kuomba au kutoa mafunzo ya kidini.
Nyimbo za Kisiasa
Hizi ni nyimbo za kuwasifia viongozi wa kisiasa
Nyimbo za Kizalendo
Nyimbo za huonyesha uzalendo kwa kusifia taifa/nchi
Nyimbo za Mapenzi
Katika nyimbo za mapenzi, mwimbaji huimba kwa kumsifia mpenzi wake hasa kwa urembo na tabia zake.