Msamiati wa Malipo

Haya ni majina ya malipo yanayotolewa kwa shughuli/haja mbalimbali.

Mifano

  1. ada:
    malipo kwa mganga au hospitali
  2. fidia:
    malipo ya mtu baada ya kumkosea mwengine au kumtia gharama/hasara
  3. karo:
    malipo kwa ajili ya mafunzo (shuleni)
  4. kiingilio:
    malipo yanayotozwa watu ili kushiriki katika jambo fulani
  5. kiinua mgongo:
    malipo anayotoa mtu kama shukrani kwa jambo alilotendewa au analotaka kutendewa
  6. kodi:
    malipo kwa kutumia nyumba au kiwanja. aghalabu hulipwa kila mwezi.
  7. marupurupu:
    pesa za matumizi ya kila siku
  8. mtaji:
    pesa ambazo mtu huhitaji ili kuanzisha biashara
  9. nauli:
    malipo ya kusafiri
  10. riba:
    pesa zaidi mtu anazopata kwa kuweka pesa kwenye banki kwa muda fulani au malipo zaidi mtu anayohitajika kulipa juu ya kiasi alichochukua kama mkopo.
  11. rushwa:
    malipo yanayolipwa kinyume cha sheria ili kumfanya mtu akupendelee katika jambo fulani.
  12. ushuru:
    malipo kwa serikali