Majazi
Majazi ni mbinu ya mhusika kuwa na jina lake rasmi (jina la kuzaliwa) linaloambatana na tabia/mienendo/sifa zake. Aidha, majazi inaweza kuwa mbinu ya sanaa.
- Mhusika Bahati katika riwaya; ikiwa maisha yake yatadhihirisha kuwa na bahati nyingi; basi hiyo itakuwa ni mbinu ya Majazi.
- Mzee Tumbo Kubwa anapenda kula sana kana kwamba hashibi.
- Neema ni msichana mzuri, mpole, mpenda amani
- Mganga Kuzimu ni mganda hodari sana anayeongoza ibada za gizani katika kijiji cha Mizukani